Breaking

Saturday, 8 March 2025

WAWEKEZAJI WALIOKIUKA MKATABA RANCHI YA USANGU KUONDOLEWA

   

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti akizungmza na wawekezaji na wafugaji kwenye mashamba ya kuzalishia Mifugo na Malisho kwenye Ranchi za Taifa Usangu wakati wa Ziara yake Machi 7, 2025 Wilayani Mbarali mkoani Mbeya.
Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti akikagua mashamba ya kuzalishia Mifugo na Malisho kwenye Ranchi za Taifa Usangu wakati wa Ziara yake Machi 7, 2025 Wilayani Mbarali mkoani Mbeya.
 Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti akikagua mashamba ya kuzalishia Mifugo na Malisho kwenye Ranchi za Taifa Usangu na kushuhudia jinsi watu waliopewa mashamba hayo walivyoanza kufanya kilimo badala ya shughuliza ufugaji wakati wa Ziara yake Machi 7, 2025 Wilayani Mbarali mkoani Mbeya.
Mifugo aina ya ng'ombe inayopatikana kwenye mashamba ya kuzalishia Mifugo na Malisho ya Ranchi za Taifa Usangu wakati wa Ziara yake Machi 7, 2025 Wilayani Mbarali mkoani Mbeya.

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti akizungmza na wawekezaji na wafugaji katika mashamba ya kuzalishia Mifugo na Malisho kwenye Ranchi za Taifa Usangu wakati wa Ziara yake Machi 7, 2025 Wilayani Mbarali mkoani Mbeya.
Mwenyekiti wa Chama cha Wafugaji Bw. Mrida Mshota akizungumza wakati wa ziara ya Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti kukagua mashamba ya kuzalishia Mifugo na Malisho kwenye Ranchi za Taifa Usangu wakati wa Ziara yake Machi 7, 2025 Wilayani Mbarali mkoani Mbeya.
Wafugaji na Wawekezaji wakimsikiliza Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti akitoa msimamo wa serikali kuhusu mashamba ya serikali ya kuzalishia Mifugo na Malisho kwenye Ranchi za Taifa Usangu wakati wa ziara yake Machi 7, 2025 Wilayani Mbarali mkoani Mbeya.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.Alexander Mnyeti ameuagiza Uongozi wa Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) kuwaandikia notisi ya kuwatoa kwenye vitalu wawekezaji waliokiuka masharti ya Mkataba wa kukodisha mashamba katika Ranchi ya Usangu.

Mhe.Mnyeti ametoa maelekezo hayo Machi 7, 2025 Wilayani Mbeya  wakati wa Ziara yake Kwenye Ranchi ya Usangu ambapo amesema serikali imetoa mashamba hayo kwaajili kuzalishia mifugo na sio shughuli za Kilimo.

" Mashamba haya ni ya kwaajili ya Mifugo  lakini kuna watu walikuja kutaka kukodisha kwaajili ya kuzalisha mifugo lakini wamegeuza matumizi na sasa wanalima hili halikubaliki, Nawapa siku tatu Narco kuwaandikia notisi wote waliokiuka"alisema Mhe. Mnyeti.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha wafugaji Tanzania (CCWT) Bw. Mrida Mshota  amesema ili kuweza kunufaika na sekta ya mifugo lazima jamii ya wafugaji na wawekezaji kukubaliana na mabadiliko.

Ziara ya Mhe. Mnyeti itaendelea kesho kwa mkoa wa Rukwa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: +255 621 896 990

Pages