Breaking

Saturday 12 October 2024

TPDC Mdhamini Mkuu Mbio za Mwl. Nyerere Marathon, Mwanza

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limekuwa Mdhamini Mkuu wa Mbio za Mwl. Nyerere Marathon zilizofanyika leo Jumamosi Oktoba 12, 2024 Igoma Mkoani Mwanza. Mbio hizo zimefanyika zikiwa na lengo la kuenzi falsafa ya Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika Maendeleo na Ustawi wa Taifa letu.

Akiongea katika hafla hiyo Bw. Donald Aponde ambaye ni Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC ameeleza kuwa: -

"TPDC tunajivunia kudhamini mbio hizi kwani Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alifanya mambo mengi ikiwemo kuanzishwa Kwa TPDC (1969) ambapo hadi sasa Shirika letu linafanya vizuri kwenye shuguli za utafutaji na uendelezaji wa nishati ya mafuta na gesi asilia nchini.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: +255 621 896 990

Pages