Breaking

Tuesday 8 October 2024

DAWASA YANOGESHA WIKI YA HUDUMA KISARAWE



Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira (DAWASA) imeanza kuadhimisha Wiki ya Huduma kwa Wateja katika Mkoa wa Kihuduma DAWASA Kisarawe kwa zoezi la kutembelea wateja mtaa kwa mtaa katika Kata ya Kisarawe hususan maeneo ya Bomani na Matumbini.

Zoezi hilo la kutembelea wateja Mtaa kwa Mtaa limelenga kuwafikia wateja kwenye maeneo yao na kuwahudumia kwa kusikiliza changamoto walizonazo na kuzitatua.

Maadhisho ya wiki ya huduma kwa wateja hufanyika kila mwaka kuanzia tarehe 7 hadi 11 Oktoba ambapo mwaka huu kauli mbiu inasema "Ni Zaidi ya Matarajio".



Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: +255 621 896 990

Pages