Breaking

Thursday 11 July 2024

WANAFUNZI 12 WAFARIKI AJALI YA GARI KUPINDUKA NA KUWAKA MOTO

Watu 13 wamethibitishwa kufariki kufuatia ajali ya kutamausha iliyohusisha basi la shule Afrika Kusini.

Kwa mujibu wa ripoti ya polisi, watoto 12 na dereva walifariki papo hapo baada ya basi hilo lililokuwa likiwapeleka shuleni kubingiria karibu na Johannesburg.

Taarifa za awali zinasema basi hilo lilipinduka na kuwaka moto baada ya kugongwa na gari lingine.

Dereva wa basi hilo pia alipoteza maisha huku watoto wengine saba wakikimbizwa hospitalini, kulingana na maafisa katika jimbo la Gauteng la Johannesburg.

"Basi dogo la uchukuzi la mwanachuo lilipata ajali mbaya eneo la Kokosi-Wedela huko Merafong na kusababisha vifo vya wanafunzi 12 na dereva wao na kuteketea kwa moto kadri ya kutoweza kutambulika," polisi wa trafiki wa eneo hilo walisema.

Picha zilizosambazwa kutoka eneo la ajali zilionyesha hali ya kusikitisha ya tukio hilo.

Taarifa ya Wizara ya Elimu ilionyesha kuwa ajali hiyo ilihusisha wanafunzi kutoka Shule ya Msingi ya Rockland na Laerskool Blyvooruitsig.

Maafisa hao walisema watoto saba walijeruhiwa na walikimbizwa katika vituo vya matibabu vilivyokuwa karibu.

Timu ya usaidizi wa kisaikolojia na kijamii itatumwa kwa shule hizo mbili ili kutoa usaidizi wa haraka na kufanya kazi kwa karibu na shule na familia zilizoathirika.

"Kupoteza watoto wetu ni pigo kubwa kwa jamii yetu, na mawazo na sala zetu ziko pamoja na familia za waliofariki na wanafunzi waliojeruhiwa," Waziri wa Elimu wa Gauteng Matome Chiloane alisema.


Source : Tuko News 

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: +255 621 896 990

Pages