Mhe.Kihongosi ametoa agizo hilo alipokuwa akisikiliza kero za Wananchi katika Kata ya Mwabuma Wilayani Meatu katika ziara yake ya ukaguzi wa Miradi,kusikiliza na kitatua Kero za Wananchi.
Aidha amemuagiza uongozi Wilayani Meatu kuhakikisha Wanasimamia kwa karibu utatuzi wa changamoto ya Maji na Umeme katika Kata ya Mwabuma kiujumla
Wananchi wa Mwabuma wamemueleza Mkuu wa Mkoa Kihongosi kuwa kukosekana kwa umeme na Maji katika Shule ya Sekondari Mwabuma kumeathiri kwa kiasi kikubwa Wanafunzi kimasomo.
Mkuu wa Mkoa Kihongosi yuko katika ziara Wilayani Meatu kwa ajili ya ukaguzi wa Miradi na kusikiliza kero mbalimbali za Wananchi.
SIMIYU-RS
01 Julai 2024.



