Breaking

Thursday 4 July 2024

"HUDUMA BORA IWE KIPAUMBELE KWA WANANCHI" - WAZIRI AWESO



Waziri wa Maji, Mhe.Jumaa Aweso (Mb) amewaelekeza Watumishi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA) kutimiza wajibu wao kwa kutoa huduma bora zinazokidhi mahitaji ya Wananchi wanaowahudumia.

Waziri Aweso ameyasema hayo katika kikao kazikazi na Watumishi wa mikoa ya kihuduma DAWASA Mbagala na Temeke wakati wa muendelezo wa ziara yake ambapo ameelekeza uboreshaji wa huduma kwa wateja pamoja na kuongeza maunganisho ya huduma kwa wateja.

Mhe Aweso anaendelea na ziara yake Mkoani Dar es salaam iliyolenga kukagua uzalishaji na usambazaji Majisafi pamoja na uhakika wa upatikanaji wa huduma kwa Wananchi





Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: +255 621 896 990

Pages