Breaking

Monday 19 February 2024

KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DK. NCHIMBI ATUA KAGERA, MAZISHI YA BALOZI DK. DEODORUS KAMALA

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi, akiwa katika mazungumzo na baadhi ya viongozi wa Chama na Serikali wa Mkoa wa Kagera, baada ya kuwasili na kupokelewa katika Uwanja wa Ndege wa Bukoba, mkoani Kagera, leo Jumatatu, Februari 19, 2024, kwa ajili ya kushiriki mazishi ya Balozi (mstaafu) Dk. Deodorus Buberwa Kamala, anayetarajiwa kuzikwa kesho Jumanne, Februari 20, 2024, kijijini kwake Bwanjai, Wilaya ya Misenyi, mkoani humo.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi, akipokelewa na kusalimiana na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali, alipowasili Uwanja wa Ndege wa Bukoba, mkoani Kagera, leo Jumatatu, Februari 19, 2024, kwa ajili ya kushiriki mazishi ya Balozi (mstaafu) Dk. Deodorus Buberwa Kamala, anayetarajiwa kuzikwa kesho Jumanne, Februari 20, 2024, kijijini kwake Bwanjai, Wilaya ya Misenyi, Mkoa wa Kagera.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: +255 621 896 990

Pages