Breaking

Wednesday 15 November 2023

DC MKUDE ATOA WITO MAKAMPUNI YA ULINZI

Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude amefunga mafunzo ya jeshi la akiba (Mgambo) tarehe 14/11/2023, katika viwanja vya shule ya Msingi Idukilo, kata ya Idukilo mafunzo yaliyojumisha wahitimu 224 wanawake 17 na wanaume 207.

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo Mheshimiwa Mkuu wa wilaya ametoa pongezi na shukrani kwa viongozi wa kata ya Idukilo kwa kuhakikisha mafunzo ya jeshi la akiba "Mgambo" yameanza na kumalizika salama, Pia amewashukuru Wakufunzi waliohusika kutoa mafunzo na kuwafanya wanafunzi kuhitimu mafunzo hayo kwa viwango vinavyohitajika.

" Ninawapongeza na kuwashukuru sana wakufunzi wote mliotoa mafunzo haya ya viwango vinavyohitajika, wahitimu wote mkawe mstari wa mbele katika kuilinda, nchi yenu na kuwa mstari wa mbele kujitolea kazi mbalimbali za ujenzi wa Taifa,

Vilevile mafunzo mliyoyapata yakawe ni sehemu ya kupeleka elimu kwa jamii juu ya maadili mema, ikiwa ni pamoja na kushirikiana na vyombo vya Ulinzi na usalama katika kutoa taarifa za uhalifu popote pale unapotokea." Alisema Mkude

Aidha Mheshimiwa Mkude ametoa wito kwa makampuni yote ya ulinzi wilayani kuajiri vijana waliopitia katika mafunzo ya Jeshi la Akiba (Mgambo) na kuwapa kipaumbele katika nafasi za Jeshinla Kujenga Taifa ( JKT ).

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Kishapu Ndugu. Emmanuel Johnson amewapogeza sana wahitimu pamoja na wakufunzi kwa kumaliza salama mafunzo pamoja na kuahidi kutenga bajeti kupitia Mapato ya ndani kwaajili ya sare za Jeshi la akiba

Naye Kamanda wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Kishapu Bi. Esther Gesogwe Amewataka wahitimu wote kuhakikisha usalama maeneo yote amabayo watakuwepo na kushirikiana kwa ukaribu na Jeshi la Polisi pamoja na kuimarisha Amani.




Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: +255 621 896 990

Pages