Breaking

Friday 18 March 2022

RAIS SAMIA ATOA POLE, MAAGIZO AJALI ILIYOUA WATU 22 MOROGORO



Na Samir Salum - Lango la habari 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesikitishwa na ajali ya basi iliyoua Watu 22 huku  32 wakijeruhiwa ajari iliotokea eneo la melela kibaoni barabara ya iringa-morogoro baada ya basi la kampuni ya Ahmed likitokea Mbeya kwenda Tanga kugongana na Lori la lilikokuwa likisafiri kwenda nje ya nchi.

Soma Zaidi AJALI YA BASI YAUA 22 NA KUJERUHI 38 MOROGORO

Ajali hiyo imetokea leo Ijumaa Machi 18, 2022 majira ya saa 11 jioni, eneo la Melea Jibaoni, njia panda ya Kilosa katika barabara kuu ya Morogoro - Iringa na kusababisha vifo vya wanaume 15 wanawake 6 na mtoto mmoja wa kiume.

Rais Samia amevitaka vyombo vyote vinavyosimamia usalama barabarani kuongeza juhudi ya kuthibiti ajali na kuwaasa madereva kuzingatia sheria.

Aidha ametoa salamu za pole kwa wafiwa na anaugana na familia hizo katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.



Soma Zaidi AJALI YA BASI YAUA 22 NA KUJERUHI 32 MOROGORO

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: +255 621 896 990

Pages