Breaking

Friday, 4 March 2022

RADI YAUA WATU SABA - KATAVI




Watu saba wakiwemo watano wa familia moja Mkoani Katavi wamefariki baada ya kupigwa na radi.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo mbele ya waandishi wa habari leo Ijumaa Machi 4, 2022 Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi, ACP Ally Makame ameelezea kuwa tukio la watu watano wa familia moja limetoka Machi 2, 2022 majira ya usiku wakiwa wamelala.

Amesema kuwa wakazi hao ni wa wa Kijiji cha Kamsisi Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi.

“Waliopoteza maisha ni Masalu Sengule (32) Muri Shija (25) Nkiya Masalu (7) Vumi Masalu (5) na Mariam Masalu umri wa miezi mitano” amesema ACP Makame

Aidha, Kamanda Makame amesema kuwa watu wengine wawili wakazi wa Mlibanzi wilayani Tanganyika mkoani humo wamefariki kwa kupigwa na radi wakiwa shambani.

Amewataja marehemu hao kuwa ni Elizabeth Nywandwi (13) na Faineth Mihani (37)”.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: +255 621 896 990

Pages